Friday 11 August 2017

Malinzi na Mwesigwa Hali si Shwari, Waendelea Kusota Jela.

Kesi inayowakabili viongozi wa nafasi za juu katika Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na Selestine Mwesigwa imehairishwa mpaka Agosti 24 mwaka huu ambapo watarudishwa tena Mahakamani kusomewa mashtaka yao.

Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu Jijini Dar es Salaam, Wilbard Mashauri, ambapo ndipo mashtaka hayo yalifunguliwa mara ya kwanza na kuendelea kusomewa mpaka sasa.

Hata hivyo, Wakili wa utetezi, Nehemiah Nkoko amedai kwamba inaonyesha vielelezo tayari vimeshafikishwa Mahakamani lakini upande wa mashtka unachelewesha kutolewa uamuzi.

Kwa upande mwingine, viongozi hao wanatuhumiwa na makosa mbalimbali  yakiwemo ya matumizi mabaya ya madaraka waliyokuwa nayo katika uongozi wao pamoja na kughushi na kutakatisha fedha kupitia akaunti ya TFF.


Toa Maoni yako Hapa Chini:

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment