Saturday 12 August 2017

Korea Kaskazini: CIA wamepanga kumuua Kim Jong-un.

Serikali ya Korea Kaskazini imesema kuwa imepata taarifa kutoka wizara ya ya mambo ya ndani yaKorea Kusini kuwa mawakala wa kundi la kigaidi linaloungwa mkono na Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) na shirika la ujasusi la Korea Kusini wameingia nchini humo kwa lengo la kumuua rais wa nchi hiyo.

Korea Kaskazini imesema kuwa kabla ya kutekelezwa kwa azmio hilo itahakikisha inawasaka mawakala hao na kuwaangamiza bila huruma

Imeyasema hayo wakati wasiwasi ukiongezeka kati ya Marekani na Korea Kaskazini dhidi ya tuhuma za matumizi ya silaha za nyuklia.

Aidha, shirika la habari la Korea Kaskazini limesema kuwa njama hiyo inahusisha kutumiwa kwa silaha kali ya bio-kemikali pamoja na kemikali yenye miale ya sumu.

Hata hivyo, mwishoni mwa wiki, Rais Marekani Donald Trump alisema anatamani kukutana na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un, ili waweze kufanya mazungumzo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment