Tuesday 15 August 2017

'Zimbabwe' ya R.O.M.A Yazidi Kuwagusa Wengi ..Nikki Mbishi Ampa Pongezi R.O.M.A.

Rapper huyo amesema ngoma hiyo ndani ya siku mbili kupata viewers zaidi 450,000 katika mtandao wa YouTube ni ishara ya kufanya vizuri na ni mafanikio katika level ya muziki wa hip hop hususani Tanzania.

Nikki ameendelea kueleza kuwa alipoona ngoma hiyo kwa mara ya kwanza alishawishika na ikabidi atumia MB zake kwa ajili ya kudownload na alipoupa na kuusikiliza alishtuka kidogo na kuhisi mbona kama jamaa kuna kitu anataka kukisema.

“Nikagundua maswali mengi siku ambao waandishi wa habari walikwenda na makamera kwenda kuhoji pale lakini yale maswali waliyomuuliza Roma siyo ambayo yalitakiwa aulizwe na ambayo waliulizwa hayakujibiwa, lakini Roma amefanikiwa japo kwa kifupi kuyajibu kwenye wimbo, kwa hiyo ni kile kila mtu alikuwa anatamani kujua,” ameiambia Planet Bongo ya EA Radio na kuongeza.

“Sijui ripoti ya utekaji ameiteka mtekaji na vitu kama vile, then anawashukuru watu waliotabiri atatoka jumapili kwa kuwa kuna manabii wametabiri kwamba mwanenu amepotea lakini jumapili atakuwa amepatikana ni vitu ambavyo ni live yeye kaviongea, me naona alichosema ni kizuri,” amesema Nikki.

Pia Nikki amesema wimbo haupo negative tu kwamba Roma anaipinga serikali kwani kamsifia Mh. Rais Dkt. Magufuli kwa kujenga bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Tanga.


Toa Maoni yako Hapa Chini:

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment