Tuesday 22 August 2017

Korea Kaskazini Yatishia Kujibu Zoezi la Kijeshi la Marekani.

Korea Kaskazini imetishia kujibu vikali zoezi la pamoja la kijeshi lililofanywa na majeshi ya Korea Kusini pamoja na yale ya Marekani.
Msemaji wa jeshi kutoka Kaskazini alisema kuwa anatazama kwa makini kile ilichokitaja mchezo wa kivita wa Marekani .

Pyongyanga imetishia kurusha makombora katika bahari ya kisiwa cha Guam ambacho kina kambi kubwa ya wanahewa wa Marekani .

Wasiwasi huongezeka wakati wa zoezi hilo la pamoja la kila mwaka, na kwamba hali imezidi kuwa mbaya zaidi baada ya Korea Kaskazini kufanyia majaribio kombora lake la masafa marefu linaloweza kushambulia Marekani.
Mwaka uliopita Pyongyang ilijibu zoezi hilo la kijeshi kwa kufanyia majaribio kombora lake.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment