Sunday 12 June 2016

PLUIJM HATAKI UTANI, BAADA YA SAFARI YA SAA 9 HADI ANTALYA, YANGA IMETUA NA MOJA KWA MOJA IMEANZA MAZOEZI.Fahamu zaidi hapa.

Kocha wa Yanga, Hans van der Pluijm, hataki mchezo na anajua ugumu wa michuano ya Kombe la Shirikisho hatua ya robo fainali.

Ndiyo maana baada ya timu yake kusafiri kwa saa takribani tisa kutoka Dar es Salaam hadi Istanbul ambayo ni saa 7 na dakika 20, halafu kutoka Istanbul hadi Antalya safari ya saa 1 ana dakika 20. Walipotua tu, wamepumzika kidogo na kuanza mazoezi.

Kikosi cha Yanga kimeanza mazoezi ingawa yalikuwa mazoezi mepesi.

0 comments:

Post a Comment