Tuesday 30 August 2016

HII NDO Hoteli mpya Tanzania, wateja hulipa shilingi milioni 22 kwa usiku mmoja.Fahamu zaidi hapa.

Hoteli hii iko katika kisiwa cha Thanda kusini mwa Tanzania. Ina vyumba 5 vya kulala ambapo itakugharimu shilingi milioni 22 kulala hapo kwa usiku mmoja.

Hoteli hii inaakadiriwa kuwa na ukubwa wa ekari 20 ikiwa imezungukwa na viumbe mbalimbali wakuvutia waliomo ndani ya maji. Hoteli hii inapakana na kisiwa cha Mafia, unaweza kufika kwa kutumia helikopta kutokea Dar es Salaam, au kwenda kwa ndege hadi Mafia na kisha kutumia boati maalum kwa ajili ya wateja.

Ukiwa katika hoteli hii unaweza kufurahia mambo mbalimbali kama kuogelea, uvuvi, diving. Hoteli hii inamilikiwa na Christin na Dan Olofsson kutoka nchini Sweden. Walikuwa na ndoto za kutafuta eneo ambalo halijakaliwa na watu na kutengeneza sehemu tulivu ya kupumzika, na ndipo wakalipata eneo hilo Tanzania.

0 comments:

Post a Comment