Monday 29 August 2016

#YALIYOJIRI>>>Polisi Wamevamia Kikao cha Ndani cha Kamati Kuu ya CHADEMA.Fahamu zaidi hapa.

Kikao cha Kamati Kuu (CHADEMA) Kinachofanyika Dar es salaam kimevamiwa na polisi na viongozi walioko meza kuu wa natakiwa kwenda polisi.

Kikao hicho kilikuwa kinafanyika katika Hoteli ya Giraffe iliyopo Mbezi Jijini Dar.

=> Muda mfupi uliopita Mwenyekiti wa Chama Freeman Mbowe, Naibu Katibu Mkuu Bara John Mnyika, Katibu Mkuu Vincent Mashinji na Mjumbe wa Kamati Kuu Edward Lowassa watakiwa polisi.

Msafara huo uko Njiani unaelekea Polisi kituo Kati baada kutaka kikao cha kamati kuahirishwa kwamba vikao na mikutano vimezuiliwa.

0 comments:

Post a Comment