Friday 26 August 2016

#BURUDANI>>>Gharama ya Video ya Saka Hela ya Nay ni Sawa na Passo 7 Mpya!...Fahamu zaidi hapa.

Baada ya kukaa kimya bila kutaja kiasi cha fedha alichotumia kushoot video yake ya ‘Saka Hela’ Nay Wa Mitego amefunguka rasmi kwa mara ya kwanza.
Rapper huyo amekiambia kipindi cha ‘Ngaz kwa Ngaz’ kinachoruka kupitia EATV kuwa ametumia kiasi cha $25,000 kushoot video yake hiyo ambazo kwa hela za kibongo ni zaidi ya shilingi milioni 50. Kiasi hicho cha fedha kinaweza kununua gari aina ya Passo mpya kutoka show room, saba na chenji inabaki!

Mpaka sasa wimbo huo una zaidi ya miezi mitatu tangu alipouachia mwezi Mei mwaka huu kwa kushtukiza na umefanikiwa kutazamwa kwa zaidi ya mara laki nne kwenye mtandao wa Youtube.

0 comments:

Post a Comment