Wednesday 31 August 2016

#MICHEZO>>>>ASAMOAH GYAN AKWAMA KUJIUNGA NA KLABU YA ENGLAND.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Uhamisho wa mkopo wa muda mrefu (msimu mmoja) wa hodha wa Ghana Asamoah Gyan kuhamia klabu ya Reading inayoshiriki ligi daraja la kwanza (Championship) umekwama.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu ya Sunderland alitarajiwa kujiunga na The Royals akitokea klabu ya Shanghai SIPG ya nchini China.

Kwa mujibu wa BBC, Gyan, 30, hatajiunga tena na klabu hiyo baada ya ripoti kutoka kwamba amefeli vipimo vya afya

Gyan alifunga magoli 10 kwenye Premier League wakati akiitumikia klabu ya Sunderland kabla ya kwenda kucheza soka kwenye falme za Kiarabu.

0 comments:

Post a Comment