Sunday 22 January 2017

Chadema Walianzisha ..!!!!..Fahamu zaidi hapa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko, Juma Maganga amepewa siku saba kueleza sababu ya kupitisha bajeti ya mwaka 2017/18 ikidaiwa ni  kinyume na utaratibu.

Wakizungumza na waandishi wa habari, madiwani kutoka Chadema walidai kuwa mwenyekiti huyo alitumia mabavu kupitisha bajeti ambayo haijakamilika.

Katibu wa madiwani hao, Medas Amosi alisema: “Mwenyekiti alienda kinyume na kifungu cha 183 cha Sheria namba 7, na kifungu 97 cha  Sheria namba 8 ya mwaka 1982  zinazotoa madaraka na mamlaka kwa Serikali za Mitaa.” 

Amosi alisema utaratibu unaotumika kupitisha bajeti ni theluthi ya wajumbe ambao huwa  12, lakini mwenyekiti huyo aliipitisha baada ya wajumbe 10 ambao ni wa CCM kuikubali, huku wanane wa Chadema wakiikataa.


Download  Application ya Hebron Male Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment