Monday 23 January 2017

Shilole Awafungukia Wanaolalamika Hali Ngumu.Fahamu zaidi hapa.

Msanii wa muziki wa bongo fleva Zuhena Mohammed alimaarufu kama Shilole amefunguka na kuwapa neno baadhi ya vijana ambao wamekuwa wakilalamika juu ya hali ngumu ya maisha huku wengi wao wakiitupia lawama Serikali ya awamu ya tano.

Shilole kupitia mtandao wake wa Instgram amesema amewachana baadhi ya vijana hao na kusema wamekuwa wakilalamika kuwa kuna hali ngumu ya maisha au pesa haipatikani ikiwa wao wenyewe hawahitaji kujishughulisha wamebaki kukaa vijiweni pasipo kuhangaika kutafuta mishe za hapa na pale za kuingiza kipato.
“Unalalamika hali ngumu huku umekaa” aliandika Shilole  ambae yupo mikoa ya kanda ya ziwa akifanya shows.
Baadhi ya mashabiki wa Shilole wamemuunga mkono kutokana na kauli yake hiyo huku wengine pia wakionyesha kutokubaliana naye wakiendelea kusema kweli maisha ya sasa ni magumu na mishe hakuna.
Shilole na Nuh Mziwanda wakifanya show ,Geita

eatv.tv



Download  Application ya Hebron Male Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment