Monday 30 January 2017

DIMITRI PAYET JEURI SANA, AKAMILISHA DILI LA UHAMISHO, AWATOLEA KAULI WEST HAM.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Dimitri Payet ametangazwa rasmi kuwa mchezaji wa Marseille ya Ufaransa akitokea West Ham United ya England kwa ada ya pauni 25m lakini kuna neno ametoa kuhusu timu yake ya zamani.
Payet ambaye alitolewa lugha nyingi kali na mashabiki wa West Ham walimuona kama msaliti kwa kugoma kucheza akitaka auzwe amesaini mkataba wa miaka minne na nusu na klabu yake hiyo ya nyumbani na kuamua kuzungumzia kilichotokea.

 Akizungumzia kuhusu tabia yake iliyojitokea mpaka dili hilo linakamilika, Payet amesema: "Sina haja ya kuthibitisha au kufafanua kuhusu tabia yangu. Slaven Bilic (kocha wa West Ham) tulizungumza na tunajua kilichotokea.

“Sina cha ziada kuzungumzia kuhusu suala hilo, naona bora nitahifadhi hayo, nitayazungumza siku nyingine lakini siyo sasa, kwa ufupi nilihitaji sana kurejea Ufaransa hasa Marseille."



Download  Application ya Hebron Male Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment