Monday 23 January 2017

Live Bila Chenga..!!Mtoto wa Mbunge Anaswa Usiku na Golikipa wa Timu ya Mtibwa Sugar Wakipeana Mahaba Mazito+Pichazz.Fahamu zaidi hapa.

Binti wa aliyekuwa Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Shaa (CCM), Naima Shaa amezua balaa kwa mara nyingine baada ya kunaswa akijiachia kwa mapozi ‘tata’ na golikipa namba moja wa Timu ya Mtibwa Sugar, Saidi Mohamed ‘Nduda’.
 Tukio hilo lililoacha gumzo kwa muda lilijiri katika Ukumbi wa Maisha Basement, Kijitonyama, Dar ambapo wawili hao walikuwa wamekwenda kustarehe.


Kwa kamera ya shushushu wetu, Nduda alifika ukumbini hapo akiwa na washkaji zake na Naima naye alikuwa kivyake lakini walipokutana hali ilibadilika na kuanza kufanya yao.
                                     Naima Shaa akiwa na Manyika JR
“Walionesha kama watu waliomisiana kitambo. Nduda alipomuona Naima tu, alimfuata harakaharaka na kuanza kupiga naye mapicha tata kabla ya kukumbatiana na kuzungumza kwa muda huku wengine wakisema kuwa ni mrithi wa aliyekuwa mpenzi wa mwanadada huyo ambaye ni kipa wa Simba, Peter Manyika Jr,”

 “Baada ya kujiachia kwa mapichapicha, wawili hao walipoulizwa kama kwa sasa ni wapenzi hawakuwa tayari kufunguka.
 alifunguka shushushu wetu na kuongeza:“Zaidi sana waliendelea kuburudika kwa muda kabla ya mwishoni kabisa kutokana na wingi wa watu waliokuwemo ukumbini hapo, haikujulikana mara moja kama waliondoka pamoja.”
Naima ambaye aliwahi kuwa mke wa mfanyabiashara wa jijini Dar, Mwanamboka, aliwahi kuripotiwa kumzidi kete aliyekuwa shosti wake, Wema Isaac Sepetu na kudaiwa kumpora kigogo wake aliyekuwa maarufu kwa jina la CK.Mbali na hilo, pia aliwahi kuripotiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na msanii wa Bongo Fleva, Aslay Isihaka ‘Dogo Aslay’ hadi kujichora tatuu ya msanii huyo. Baada ya kuachana na Dogo Aslay, Naima alitumbukia kwenye penzi la Peter Manyika Jr kabla ya uhusiano wao kukata kamba miezi kadhaa iliyopita.


Download  Application ya Hebron Male Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment