Sunday 29 January 2017

MANE AIMWAGA SENEGAL NJE YA AFCON, AKOSA PENALTI YA MWISHO, CAMEROON YASONGA NUSU FAINALI.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Senegal iliyokuwa inapewa nafasi kubwa ya kubeba ubingwa wa Afcon, imetolewa katika hatua ya robo fainali na Simba Wasioshindika, Cameroon wamesonga mbele.

Cameroon wamesonga mbele baada ya ushindi wa penalti 5-4, penalti ya mwisho ya Senegal ilipotelea kwa nyota wake Sadio Mane anayekipiga katika kikosi cha Liverpool nchini England.

Kwa Liverpool itakuwa furaha kuu maana bila Sane mambo yalionekana yanakwenda kombo. Lakini kwa Wasenegali ni majonzi makubwa wakiwa wanaenda nyumbani.

Katika mechi hiyo, dakika 90 halafu 120 ziliisha kwa sare ya bila mabao huku Senegal ikiwa imepoteza nafasi nyingi za kufunga.

 PENALTI ZILIVYOKUWA
SENEGAL
Koulibaly - FUNGA
Kara - FUNGA
Sow -FUNGA
Saivet - FUNGA
Mane - KOSA 


CAMEROON
Moukandjo - FUNGA
Oyongo - FUNGA
Teikeu - FUNGA
Zoua - FUNGA
Aboubakar - FUNGA
Senegal (4-3-3): Diallo; Gassama, Kara, Koulibaly, M'Bengue (Ciss 86mins); Gueye, Saivet, Kouyate (Ndiaye 109); Mane, Diouf (Sow 64), Keita.
Booked: Diouf, Kouyate.


Cameroon (4-3-3): Ondoa; Fai, Teikeu, Ngadeu-Ngadjui, Oyongo; Siani, Moukandjo, Djoum (Mandjeck 102); Bassogog, Tambe (Aboubakar 102), Ekambi (Zoua 46).

Booked: Oynogo, Fai, Djoum.
Download  Application ya Hebron Male Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment