Desemba 23, 2015 Kiongozi wa dhehebu la
kiislamu la Shia Ithna-sheriya Tanzania Sheikh Hemedi Jalala kuhusu
kutoa mkono wa heri ya Krismasi alinukuliwa akisema “Lazima
tutambue kuwa binadamu wote ni ndugu ambao tumetokana na kizazi cha
Adam na Hawa, na hivyo hakuna sababu za kuuvunja undugu huo
hata katika imani waislamu na wakristo wana amini kuwa Mungu ni mmoja na ipo siku ya hesabu ipo, na hivyo kitendo cha kuonana katika imani moja ni moja ya sababu kubwa ya kushirikiano” Alisema
Katika kuendeleza hilo jana jioni Sheikh
Jalala aliamua kuandaa futari ya pamoja katika msikiti wa Masjid
Alghadiir uliopo Kigogo Dar es salaam na kuialika kamati ya AMANI ya mkoa huo, Kamati inayojumuisha viongozi wa dini mbalimbali ndani ya mkoa wa huo, ambayo iko chini ya uongozi wa mwenyekiti wake Samahat Sheikh Alhady Mussa Salim (sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam).
0 comments:
Post a Comment