Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania Jaji Joseph Warioba amewataka watanzania
 wote kuungana na kujiaandaa kukabiliana na baa la njaa ambalo huenda 
likatokea, huku akikiri kuwa tatizo la upungufu wa chakula kwa mwaka 
huu, ni kubwa kuliko kawaida.
Akizungumza leo wakati akizindua kongamano la 'Wanawake na Uongozi' 
katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Dar es Salaam, Jaji Warioba amesema
 hakuna haja ya watanzania kubishana na kulumbana kama kuna njaa au 
upungufu wa chakula, bali kujiandaa ikiwa ni pamoja na kujifunza 
kujifunza katika nchi ambazo tatizo hilo limetokea ikiwemo Kenya na 
Somalia.
"'Haijalishi kama njaa ipo au kuna upungufu wa chakula kinachotakiwa ni 
kuungana  na kujiandaa kwa pamoja ili kujua ni jinsi gani tutaweza 
kukabiliana na baa la njaa endapo litatokea kama jinsi inavyosemwa, 
tujifunze kupitia Kenya na Somalia. Siyo sawa kurushiana maneno huyu 
anasema hivi huyu anamjibu vile, tuungane kwa pamoja" Amesema Warioba 
ambaye pia alikuwa ndiye Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba a 
kuongeza “Serikali ijiandae kukabiliana na njaa kwa sababu ingawa 
tumezoea kwamba kila mwaka zipo sehemu zenye upungufu wa chakula, mwaka 
huu tatizo ni kubwa”
Kuhusu vita dhidi ya dawa za kulevya, Warioba ametaka elimu itolewe kwa 
watu wanaojishughulisha na dawa za kulevya hususani wanaolima bangi 
lakini pia wasaidiwe wapate njia mbadala za kuweza kujikimu ili kuachana
 na shughuli hizo ambazo zinaathiri asilimia kubwa ya vijana.
Ameongeza kuwa tatizo la dawa za kulevya linaripotiwa kawaida kama siyo tatizo kwa sababu limefanywa kama jambo la siasa.
"Tatizo la dawa za kulevya linazungumzwa kama jambo la kawaida, badala 
yake tumetafuta mchepuo wa kisiasa, ambao ndiyo unazungumzwa, Karibu 
kila siku utaona taarifa kwamba wameenda askari wameharibu dawa za 
kulevya katika mashamba ya bangi, inaripotiwa tu kama tukio halafu 
basi. 
'Tuseme hapana matumizi ya madawa, madawa ni mengi sana yanayoingia , 
tunajua madhara yake, tuyazuie yanayoingia kutoka nje pamoja na 
yanayolimwa, tujitahidi kuwasaidia vijana walioathirika. Tunahitaji 
kujenga nguvu za pamoja" Amemalizia jaji Warioba.
Kongamano hilo lililoandaliwa na Mtandao wa Wanawake na Katiba, ni 
sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, na limetumika pia 
kuzindua kitabu chenye jina 'Nguvu zetu, Sauti zetu, Ajenda katika 
mchakato wa katiba mpya' kilichoandaliwa na mtandao huo jijini Dar es 
salaam, 
Download Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa
Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
 









 




 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment