Home »
Michezo
» #MICHEZO>>>MEDEAMA SC YA GHANA YAJIPANGA KUIKIMBIA YANGA.Fahamu zaidi hapa.
Taarifa kutoka Ghana zinaleza kuwa, wapinzani wa Yanga katika kundi A
Medeama SC iko mbioni kujitoa kwenyemichuano ya Shirikisho Afrika
kutokana na kukumbwa na ukata mkubwa. Hii ni kwa mujibu wa Meneja Tawala
wa klabu hiyo Bejamin Kessie.
Klabu hiyo yenye maskani yake maeneo ya Tarkwah wanataraji kucheza na
TP Mazembe-Congo katika mchezo wao wa awali hatua ya makundi
utakaopigwa June 17 jijini Lubumbashi.
Hata hivyo, Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) bado halijatoa
fedha za kujikimu kwa klabu zote zinazoshiriki michuano hiyo, hivyo
Medeama kukosa fedha zitakazowezesha safari nzima ya kwenda nchni Congo.
“Kwa sasa klabu haina fedha na inahitaji msaada mkubwa. Kwa maana
hiyo tunafikiria kujitoa kwenye michuano hii endapo hatutapa msaada
wowote,” ilieleza taarifa kutoka ndani ya klabu.
Kifungu cha 13 cha kanuni za CAF kinaeleza kuwa: “Endapo klabu
itajitoa kabla ama wakati wa 8 bora, itapata adhabu ya kupigwa faini ya
dola 1500 vile vile kukosa fedha za kijikimu zinazotolewa na CAF
(engagement fees).”
“Mbali na adhabu hiyo, vile vile itakumbwa na adhabu ya kuzuiliwa ama
kufungiwa kushiriki michuano yoyote ya CAF kwa kipindi cha miaka mitatu
kutokana na kujitoa huko.”
Mwaka 2012, klabu nyingine ya Ghana Nania FC, ambayo inamilikiwa na
legend wa taifa hilo Abedi Pele, ilijitoa kutokana sababu hizo hizo.
Nania, ambayo maskani yake ni Legon pia walipata fursa ya kushiriki
michuano hiyo baada ya kushinda kombe la FA nchini humo, kama ambavyo
Medeama ilivyopata nafasi hiyo.
Related Posts:
#MICHEZO>>>USAJIRI Mchezaji wa timu ya Chelsea kutimkia Juventus.
Nemanja
Matic kutimkia Juventus,Inasemekana Chelsea Wameafikiana makubaliano ya
paundi milioni 20 na mabingwa hao wa Serie A.Kocha anaekuja kuchukua
mikoba ya Hiddink,muitaliano Conte hajaridhika na mchezaji huyo kubaki
… Read More
#MICHEZO>>>Harry Kane wa Tottenham Hotspurs donge nono lamtembelea.Fahamu zaidi hapa.
Mshambuliaji
raia wa Uingereza Harry Kane 22,huenda akazawadiwa kwa mkataba mnono na
klabu yake ya Tottenham Hotspurs kutokana na msimu mzuri.Mshambuliaji
uyo anaelipwa paundi 50,000 kwa wiki atalipwa mara mbili ya msha… Read More
#MICHEZO>>>SAMATTA AREJEA UWANJANI GENK IKIZIDI KUTISHA LIGI KUU UBELGIJI.Fahamu zaidi hapa.
KIKOSI cha KRC Genk
anachochezea nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta leo
kimeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Zulte-Waregem kwenye mchezo
wa ligi kuu nchini Ubelgiji.
Genk walipata bao la
kwanz… Read More
#MICHEZO>>>WAAMUZI KUTOKA GHANA KUAMUA MECHI YA YANGA CAF.Fahamu zaidi hapa.
MWANDISHI WETU
Mwamuzi Joseph Odartei Lamptey,
Jumamosi Mei 7, 2016 anatarajiwa kuwa mwamzi wa kati katika mchezo wa
kimataifa kuwania Kombe la Shirikisho Barani Afrika utakaozikutanisha
timu za Young Africans ya Dar… Read More
#MICHEZO>>>>FIFA YAILIMA FAINI SIMBA, YAPANGA KUISHUSHA DARAJA.Fahamu zaidi hapa.
SHIRIKISHO la Soka la
Kimataifa (FIFA), limeipiga faini ya Franc 2,000 za Uswisi (Sh
4,582,000), Klabu ya Simba baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kupuuza
maagizo ya Idara ya Utatuzi wa Migogoro (Desputes Resolution Cha… Read More
0 comments:
Post a Comment