Thursday, 11 August 2016

#BURUDANI>>>>Naj na Mr Blue wadaiwa kuwasiliana, Naj aeleza kwanini alisave namba ya Mr Blue kwa jina la ‘Zai’.Fahamu zaidi hapa.

Msanii wa muziki Naj amekanusha tetesi za kugombana na mpenzi wake Barakah Da Prince baada ya kudaiwa kupigiwa simu usiku wa manane na aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Mr Blue.

Inadaiwa wakati Barakah ameshika simu ya mpenzi wake Naj, alipiga mtu ambaye namba yake ‘iliseviwa’ Zai na baada ya Barakah kupokea alikuta sio mwanamke bali ni mwanaume ambaye alidaiwa kuwa ni Mr Blue.

Akiongea katika kipindi cha U-Heard cha Clouds FM cha Jumatano hii, Naj amekiri kusave kimakosa namba ya Mr Blue kwa jina la Zai.

“Kuna watu wanaongea vibaya lakini hawajui, kwanza mimi siwasiliani na Mr Blue, unajua mimi mtu nikishakuwa naye hatuwezi kuwa marafiki, mnakuwa marafiki mnaongea nini sasa,” alisema Naj.

“Na mimi zamani sana hata kabla sijaanza mahusiano na Barakah, nikapata missed call kwenye hiyo namba, sasa mimi nikaisave ‘Zai’ kwa haraka haraka ili niingie whatsapp ili nijue ni nani, kwa sababu mimi mara nyingi nikipataga missed call sitakagi kumpigia mtu ambaye simjui, kwa hiyo baada ya kufanya hivyo ndo nikamjua ni nani. Kwa hiyo ilikuwa kitambo sana halafu mimi mwenyewe nilikuwa sijafuta wala nini na sio kwamba ni namba ambayo naitumia wala nini,” alifafanua zaidi.

Pia Naj ameeleza jinsi mpenzi wake Barakah alivyoigundua namba ya Mr Blue kwenye simu yake.

“Nilimpa Barakah simu yangu akawa anaitumia hata sijui kati yao nani alimpigia mwenzake kwa sababu namba ilikuwa kwenye majina. Kama ningekuwa na mambo mengi nisingejiamini kumpatia simu mpenzi wangu, kwa hiyo hata sijui nani alimpigia mwenzake kati yao, lakini namba ilitokea kama Zai,” alisema Naj.

Hata hivyo hivi karibuni katika kipindi cha U-Heard, rapper Mr Blue ambaye alifunga ndoa mapema mwaka huu na mwanadada aitwae Warda, alikana kuwasiliana na Naj.

Source:Bongo5

Related Posts:

  • Sakata la Diamond Kudaiwa Mil 400 na TRA lafika Hapa. Siku chache tangu Mbunge wa Jimbo la Mikumi Professa Jay kupaza sauti yake kuhusu makadirio makubwa ya kodi anayotakiwa kulipa Mwanamke anayewika nje na ndani ya nchi  katika muziki wa bongo Flavor Diamond  Pla… Read More
  • TANZIA: Dogo Mfaume Hatunaye Tena. Msanii wa muziki wa bongo fleva, Dogo Mfaume ambaye aliwahi kutamba na nyimbo kama 'Kazi Yangu Ya Dukani' amefariki dunia jana katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa akiendelea kupatiwa matibabu. Dogo Mfau… Read More
  • Wastara Awaburuza Wasambaza Filamu Bongo Kortini. STEPS Entertainments, ambayo ni kampuni ya kusambaza filamu Tanzania, imepelekwa mahakamani na Wastara Juma, anayeidai kiasi kikubwa cha fedha baada ya kukataa kumlipa, Risasi Jumamosi limeambiwa. Kwa mujibu wa chanzo, m… Read More
  • Picha: Zari atua hospital kumjulia hali ex wake Ivan.Mama watoto wa Diamond, Zari the Bosslady ameonekana katika picha akimjulia hali ex wake Ivan Ssemwanga ambaye anadaiwa kulazwa katika hospitali moja nchini Afrika Kusini baada ya kupata matatizo ya moyo. Zari akiwa hospi… Read More
  • Rayvanny afunguka mema Sugu aliyomtendea.Msanii Rayvanny amesema Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ni mtu ambaye ameshiriki kwa kiasi kikubwa katika video yake ya ‘Zezeta’ ambayo ipo mbioni kutoka. Rayvanny Rayvanny amesema Sugu ndiye alimpa idea … Read More

0 comments:

Post a Comment