Mwanafunzi
 wa mwaka wa kwanza, Kitivo cha Sayansi ya Jamii katika Chuo Kikuu cha 
Dodoma (UDOM), Fredrick Joseph (25), ameuawa kwa kushambuliwa kwa kipigo
 na watu wanaosadikiwa kuwa ni wanafunzi wenzake wakati akitoka klabu ya
 pombe (Bar).
Tukio
 hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana katika eneo la chuo hicho ambapo 
mwanafunzi huyo alisikika akipiga kelele ndipo walinzi wakafika na 
kumkuta akiwa anagalagala njiani.
Akizungumzia
 tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa, amesema
 mwanafunzi huyo ambaye ametokea Musoma mkoani Mara alishambuliwa kwa 
kupigwa sehemu mbalimbali za mwili wake na watu wasiofahamika.
Amebainisha
 mwanafunzi huyo alikutwa majira ya saa 10 alfajiri katika eneo hilo la 
chuo hicho huku akisema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa marehemu 
huyo alikuwa na ugomvi na watu hao katika klabu ya pombe ya Canival Pub 
iliyopo chuoni hapo.
“Alipoondoka
 kurudi bwenini akiwa njiani alishambuliwa na watu hao wasiofahamika na 
kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili wake, kipigo kilichosababisha kifo
 chake wakati alipokimbizwa kutibiwa katika Hospitali ya Rufaa ya 
Dodoma,” alisema Mambosasa
Amesema
 mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali hiyo kwa uchunguzi 
zaidi na hadi sasa hakuna mtu anayeshikiliwa kuhusiana na tukio hilo.
Alipoulizwa
 kuwa taarifa za mwanafunzi huyo kushambuliwa na wenzake, Mambosasa 
alisema kwasababu inadaiwa haifahamiki upelelezi bado unaendelea.
“Kwa
 sababu mwenye bar si yupo, kama kuna ugomvi ambao ulikuwa unaendelea 
tutajua tu, nimemuelekeza OCD kufuatilia ni nani waliokuwa wanakunywa 
kwenye hiyo bar chuoni, ni lazima tu watakuwa wanachuo ili tuwabaini,”
Kamanda huyo amesema ameelekeza uchunguzi wa kina ufanyike kama kulikuwa na ugomvi ndio hao hao walienda kumtegea njiani.
Chanzo cha habari ambacho hakikutaka kutaja jina lake kwa madai kuwa  siyo msemaji wa polisi kimesema
 kuwa marehemu Joseph alikuwa anakunywa pombe pamoja na marafiki zake 
lakini baada ya kulewa walianza ugomvi ambao hata hivyo waliamuliwa.
“Baada
 ya kuamuliwa ule ugomvi wa awali ndipo wenzake walipokwenda kumsubiria 
kwa mbele kwenye kichaka ambapo walimvamia na kumshambulia na kumwacha 
karibu ya kufa,” kilisema chanzo hicho.
Kiliongeza
 kuwa, baada ya kumwacha hapo na kutoweka ndipo walinzi wa chuo hicho 
waliokuwa doria walimuokota na kumfikisha kwenye kituo kidogo cha polisi
 kilichopo Chimwaga ambapo alikimbizwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa
 wa Dodoma alipofariki wakati akipatiwa matibabu.
Chanzo hicho kimesema hakuna mtuhumiwa hata mmoja anayeshikiliwa na polisi kwa kuwa wote waliomshambulia walitoroka na hawajulikani walipo.
 









 




 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment