Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli amesema kuwa 
baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma walioondolewa chuoni hivi 
karibuni hawakuwa na sifa za kujiunga na masomo chuoni hapo.
Akizungumza
 leo katika uzinduzi wa Maktaba mpya ya Kisasa katika Chuo Kikuu cha Dar
 es Salaam, Rais Magufuli amewataka watanzania kuweka siasa kando 
nakuzungumzia masuala ya msingi, huku akiwashangaa wanasiasa 
waliojitokeza kuwatetea wanafunzi hao.
“Nimeshukuru
 wale vijana wameondoka. Wanasiasa haohao, ‘eti ooh.. hao vijana 
wamekosa pa kulala.. it’s nonsense’. Taifa letu tuliweke mbele kwanza. 
Siasa zije nyuma,” alisema.
Alisema
 kuwa baadhi ya wanafunzi ambao walibainika kuwa na elimu ya kidato cha 
nne waliofeli masomo yao na kuruhusiwa kuendelea na masomo ya elimu ya 
juu ni watoto wa viongozi.
“Ukimchukua
 mtoto wa form four ukampeleka pale, hata kama atafanikiwa kupata 
degree… itakuwa ya ajabu. Na baadhi ya watoto waliopelekwa pale ni 
watoto wa viongozi. Watoto wa Maskini wenye qualification wamekosa 
nafasi za kwenda Chuo Kikuu. Watoto wa watu fulani fulani wanapelekwa 
wakati walifeli. It can’t be,” Dk. Magufuli alisisitiza.
Rais
 Magufuli aliongeza kuwa Serikali yake haitaruhusu fedha zinazopaswa 
kutumika kwa ajili ya maendeleo ya wananchi kupelekwa kwa ‘vilaza’ huku 
waliofaulu wakikosa mikopo ya elimu ya juu.
Dk.
 Magufuli ameahidi kuwa Serikali yake itahakikisha wanafunzi waliofaulu 
kwa kiwango cha daraja la kwanza na la pili (division 1 &2) 
wanajengewa mazingira mazuri ya kuendelea na masomo.
“Waliofeli watafute vyuo vyenye size yao,” alisisitiza.













0 comments:
Post a Comment