Thursday 18 January 2018

Aliyekuwa Meneja Wake Mtulia Naye Achukua Fomu Kugombea Ubunge Kinondoni.

Aliyekuwa meneja kampeni wa Maulid Mtulia kwenye uchaguzi wa 2015 Kinondoni, Rajabu Salim Jumaa leo Alhamisi amechukua fomu kugombea ubunge jimbo hilo.

Mwaka 2015 mgombea wa CUF Mtulia alishinda ubunge wa jimbo hilo lakini alijivua uanachama wa CUF na kuhamia CCM na hivyo kupoteza sifa ya ubunge.

Akizungumza leo Alhamisi, Juma amesema atamshinda Mtulia katika nafasi hiyo kwa sababu anaisababishia Serikali hasara.

"Gharama kubwa za uchaguzi zinasababishwa na Mtulia ambaye alishakuwa mbunge lakini amejiuzulu na kutaka tena ubunge.”

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment