Wednesday 31 January 2018

TID: Kuwa Karibu na Makonda Kumenifanya Nikose Show.

Msanii wa muziki, TID amelalamika kuwa baadhi ya watu wanamfanyia figisu figisu ili asipate show kutokana na ukaribu wake na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Muimbaji huyo amefunguka hayo katika kipindi cha Eight cha TVE kwa kudai kuwa hali hiyo inampa tabu sana.

“Kuna watu wananibania kupata dili, wengine wanaenda mpaka kwa waandaaji sipati show. Napata dabu kweli,” amesema TID.

TID ameongeza kuwa Mhe. Makonda ni mtu ambaye yuko poa sana na watu na kila anachokifanya anakuwa na uhakika nacho.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment