Wednesday 24 January 2018

Vanessa Mdee Asimulia Alichokerwa kwa Jux.

Malkia wa Bongo Fleva anayefanya vizuri ndani na nje ya nchi, Vanessa Mdee amefunguka na kuweka bayana kwamba alikuwa anakerwa na tabia ya mpenzi wake Jux ya ku-follow wanawake ambao hawaendani nae katika mitandao ya kijamii.

Vanessa ametoa siri hiyo ambayo ilikuwa inamtafuna katika moyo wake kwa kipindi kirefu kupitia kipindi cha 'Planet Bongo ya East Afrika Radio' wakati alipokuwa akifanya mapitio ya albamu yake 'Money Monday', na kusema wimbo wa unfollow ni jambo la kweli ambalo yeye mwenyewe amelipitia katika mahusiano yake na lilikuwa linamkera kupita kiasi.

"Wimbo huu ni stori ya ukweli kabisa ambapo mpenzi wangu alikuwa ananikera na tabia ya ku-follow wasichana wengine katika 'Instagram' ambao nilikuwa siwataki, siwapendi halafu hatuendani nao. Nikawa namuuliza unawa-follow wa kazi gani ? lakini sikuwa napata majibu sahihi", alisema Vanessa.

Pamoja na hayo, Vanessa amedai ameandika wimbo huo kutoka na shida wanazipitia jinsia ya kike (wasichana na wanawake) wanayoipata kwa wapenzi wao pindi wanapotumia mitandao ya kijamii.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment