Wednesday 31 January 2018

Hii Ndio Gharama ya Passport za Kielektroniki.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt.  Mwigulu Nchemba amesema kuwa gharama mpya ya hati ya kusafiria ya kielektroniki itakuwa Sh. 150,000.

Dk Nchemba amesema hayo leo  wakati wa uzinduzi wa Hati ya kusafiria ya kielektroniki jijini Dar es Salaam ambapo imezinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Aidha Dkt. Miwgulu Nchemba amesema kuwa Pasipoti hizo zitakuwa na ukurasa zaidi ya mmoja  na mwonekano mpya.

“kiasi cha gharama hiyo  ni sawa na Sh15,000 kwa mwaka kwa sababu itatumika kwa miaka 10. Gharama za kupata pasipoti sasa ni TSh.50,000 na hutumika kwa miaka 10 tangu zilipotolewa,“ amesema Dkt. Mwigulu.

Hata hivyo Rais Magufuli amesema kuwa gharama ya laki moja na nusu bei hiyo ni ya juu kidogo kuliko bei ya sasa . huku kieleza kuwa bei hiyo imezingatia ubora wa utenngenezaji wa Pasipoti hiyo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment