Thursday 18 January 2018

Maalim Seif Amtembelea Kingunge Hospitali Kumjulia Hali.

January 18, 2018 Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amemtembelea Mwanasiasa mkongwe nchini Kingunge Ngombale Mwiru aliyelazwa katika wodi ya Mwaisela, hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Maalim Seif amempa pole ya msiba wa mke wake Peras Kingunge, namnukuu Maalim “Tuwe na subira na msiba uliotufika, najua imekuumiza zaid wewe ila ndo ubinadamu sote tunaenda hukohuko, mama katangulia na sisi tunafuata,”

Mzee Kingunge aliruhusiwa kutoka hospitalini hapo Januari 10 ili kwenda kushiriki mazishi ya mkewe, Peras Ngombare Mwiru yaliyofanyika Alhamisi katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salam.

Mzee Kingunge alilazwa hospitalini hapo baada ya kushambuliwa na mbwa nyumbani kwake eneo la Victoria jijini Dar es salam hivi karibuni.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment