Tuesday 23 January 2018

Msimamizi wa Uchaguzi Kinondoni Atupilia Mbali Mapingamizi ya Wagombea Katika Jimbo Hilo.

Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Kinondoni ambaye pia mkurugenzi wa manispaa hiyo, Aron Kagurumjuli ameyatupilia mbali mapingamizi matatu yaliyowasilishwa na wagombea wa vyama vya Chadema, CCM na CUF.

Mapingamizi hayo ni kwa mgombea wa CUF, Rajab Juma kumwekea mgombea wa Chadema, Salumu Mwalimu, wakati Mwalimu yeye alimwekea Maulid Mtulia wa CCM na mgombea huyo wa chama tawala alimwekea mgombea wa SAU, Johnson Mwangosi.

Baada ya jana ofisi ya msimamizi wa uchaguzi kutoa barua ya utetezi kwa wagombea waliowekewa mapingamizi leo Jumanne imetoa majibu ya kuyatupilia mbali mapingamizi hayo.

Akizungumza na Mwananchi leo, Jumanne Januari 23, 2017, Kagurumjuli amesema “Tumeyatupilia mbali mapingamizi yao kwa sababu hayana mashiko, kilichobaki ni wagombea kwenda uwanjani wakapambane,” amesema msimamizi huyo. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment