Thursday 25 January 2018

Baada ya Kubwagwa na Heri Muziki Diva Anyapia Penzi la Soudy Brown.

Baada ya kubwagana na mpenzi wake Heri Muziki, Diva amefunguka mipango yake ya kuwa na Soudy Brown.

Mtangazaji huyo wa kipindi cha Ala za Roho cha Clouds Fm amesema kwa sasa yupo tayari kubadili dini kwa ajili ya Soudy Brown ambaye ni mtangazaji mwenzake katika kituo hicho.

“Soudy Brown ndio kila kitu kwangu niseme hivyo, urafiki wangu uko karibu kupita kiasi like hakuna kama Soudy I think he my only true love,” Diva ameiambia Bongo5.

“Kwa sababu yeye ni mtoto wa kislam akiniongeza kwenye list nitabadilisha dini na nitaitwa Amina,” amesisitiza.

Hata hivyo ameongeza kuwa tayari anamjua mpenzi wake Soudy Brown ila kitu ambacho watakaa na kujadili. Diva kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya ‘Waambie’ ambao amewashirikisha  Mr. Paul na Mwana FA.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment