Friday 19 January 2018

Ambaer Lulu Ateswa na Penzi la Young Dee Akiri Kurudiana Naye Pindi Ataachana na Prezzo.

Msanii wa muziki ambaye alijipatia umaarufu kupitia mitandao ya kijamii, Amber Lulu, amekiri kuwa bado ana hisia za mapenzi kwa mpenzi wake wa zamani rapper Young D, licha ya kuwa na mtu mwengine kwa sasa.


Amber Lulu ambaye kwa sasa yupo kwenye mahusiano na rappper wa Kenya Prezzo, amesema Young D ni mmoja wa wanaume ambaye alikuwa na mapenzi naye ya dhati, na iwapo ataachana na Prezzo yupo tayari kurudi kwa Young D, kwani anaamini hata yeye bado anampenda ndio maana huwa anamfanyia vitu vya kumuumiza kama kupost picha zAke za utupu.

“Tulishakuwa pamoja kwa muda mrefu, kuna feelings fulani zipo sometimes munamisiana, unajua nilimpenda sana D lazima kukubali hili jambo, na najua bado kuna mapenzi kati yetu ndio maana hata yeye anafanyaga vitu vya kuniumiza kama kupost ile picha”, amesema Amber Lulu.

Amber Lulu amesema tatizo hilo limefikia hatua hata ya kurushiana vijebe mitandaoni kutokana na wivu uliopo kati yao, na wapo Young D ataamua kumpost mpenzi wake mpya, kitendo hicho kitamuumiza zaidi.Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment