Friday 5 January 2018

Chege Akiri Kuathirika.

Msanii Mkogwe kutoka TMK Chege Chigunda amekiri kuwa aliathirika kisaikolojia baada ya kundi la TMK Wanaume Family kuanza kuvunjika.


Chege ametoa kauli hiyo leo akiwa ndani ya Planet Bongo ya East Africa radio na kusema kwamba boss wake ndiye aliyemtia  moyo nakumfanya azidi kupambana na kufikia mahali ambapo anapataka.

Akijibu swali la mtangazaji, Chege amesema kwamba "Nisiwe muongo kuvunjika kwa TMK Family kulinifanya niathirike kisaikolojia. Namshukuru sana Bosi wangu alinitia moyo na kuniambia kwamba nilikuwa pale kwa ajili ya kujitengeneza na siyo kumtegemea mtu aniimbie. Ujasiri wa maneno yale ndiyo yaliyonitia nguvu"

Akizungumzia kuhusu yeye na Temba kuonekana kuonekana maarufu ndani ya kundi kuliko wasanii wengine, Chege amesema kwamba kwenye kundi hakuwezi kuwa na watu maarufu wawili na kuongeza kwamba ndiyo maana yeye na Temba walibahatika.

Akizungumzia kuhusu wao wawili kuonekana na kusikika zaidi ikiwa ni pamoja na kutengeneza kombinesheni pamoja na Temba, Chege amesema kwamba muunganiko wao ulitengenezwa na wahindi ambao walipenda kazi yao na baadae kuamua kufanya kazi na muunganiko huo wa Chege na Temba.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment