Wednesday 10 January 2018

Romelu Lukaku Ahusishwa na imani za Kishirikina.

Mapya yameibuka baada ya moja kati ya matajiri wa klabu ya Everton Farhadi Moshri kuibuka na kutaja masuala ya ushirikina kuwa kati ya mambo ambayo yalimfanya Lukaku kuondoka katika klabu yao.

Farhadi Moshri amesema kwamba kilichomuondoa Lukaku kutoka Everton sio masuala ya kipesa kama inavyoonekana kwani walikuwa tayari kumpatia hadi kiasi cha £140,000 kwa wiki ila alikataa.

Lakini Moshri anadai kwamba mchezaji huyo alikuja Africa ambapo alikutana na ujumbe wa mganga ambao ulimshauri kuondoka katika klabu ya Everton na kutimkia Chelsea ambapo hata hivyo baadae alikwenda Manchester United.

Moshri amesema kwamba masuala yao na Lukaku yalikuwa yakikaribia kabisa kumalizika na hadi wakala wa mchezaji huyo alikuwa akikaribia kumaliza jambo hilo lakini ghafla Lukaku alibadilika.

Tajiri huyo wa Everton pia ameeleza masikitiko yake kuhusu Ross Barkley kwani anaamini wao kama Everton mchezaji huyo ndio waliamini anaweza kubaki nao baada ya Stones na Lukaku kuondoka ila hawakuwa na namna zaidi ya kumuuza kwenda Chelsea.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment