Wabunge nchini Afrika Kusini
wamepigana bungeni baada ya spika kuamuru maafisa wa usalama kuwaondoa
kwa lazima wabunge wa upinzani ambao walimbeza rais Jacob Zuma
alipoingia bungeni tayari kulihutubia kikao.
Hata hivyo ujio wake uliwakera sana wabunge wa chama cha upinzani Economic Freedom Fighters (EFF).
Wabunge hao chini ya kiongozi wao Julius Malema walipiga mayowe na kumtupia matusi bw Zuma jambo lililomlazimu spika wa bunge kuamuru wabunge hao wa EFF kuondolewa nje.
Ijumaa iliyopita mahakama ya juu ya Afrika Kusini iliamua kuwa rais Zuma anapaswa kufikishwa kizimbani kufuatia kesi za ufisadi dhidi yake.
0 comments:
Post a Comment