Tuesday 25 August 2015

#MICHEZO>>Balotelli akamilisha matibabu AC Milan.Fahamu zaidi hapa.

Hatimaye Mario Balotelli anaelekea kuondoka Liverpool kurudi nyumbani kujaribu maisha AC Milan kwa mkopo wa msimu mzima, baada ya kuvurunda msimu uliopita Anfield.

Mshambuliaji huyo wa kati alikamilisha vipimo vya afya Milan, ambapo atapunguziwa malipo yake kiasi, huku Liverpool wakiendelea kulipa sehemu ya mshahara wake akiwa Italia. Huenda atacheza mechi ya Jumamosi dhidi ya mahasimu wa Milan, Empoli.

“Milan wamekuwa daima moyoni mwangu na nilikuwa na matumaini kwamba siku moja ningerudi hapa. Je, nitamalizia maisha yangu ya soka hapa? Hilo litakuja baadaye, natakiwa kufanya kazi kwa bidii ili niwe na mwaka mzuri.

“ Nasubiri kwa hamu kuanza mazoezi na kuonesha watu kwamba nina thamani. Nina motisha nyingi za kufanya vizuri lakini naomba nianze kufanya kazi na si kuongea,” akasema Mtaliano huyo mtata mwenye umri wa miaka 25.

Balotelli akiwa ndiye tegemeo la Liverpool msimu uliopita alifunga bao moja tu kwenye ligi kuu nchini England, baada ya kuwa amesajiliwa kwa pauni milioni 16 kutoka Milan Agosti mwaka jana.

Hakuambatana na timu kwenye ziara ya kabla ya msimu Mashariki ya Mbali na Australia na amekuwa akifanya mazoezi nje ya kikosi cha kwanza.

Alikuwa anaonesha hapendi kuondoka Liverpool kutokana na malipo mazuri licha ya kocha Brendan Rodgers kujenga mazingira ya kumwondoa, lakini baada ya kusajiliwa kwa washambuliaji wakali, Christian Benteke, Roberto Firmino naDanny Ings, huku  Divock Origi akirejea Anfield kutoka Lille alikokuwa kwa mkopo, Balotelli ameona hana namba kabisa.

0 comments:

Post a Comment