Sunday 30 August 2015

#MICHEZO>>>Bolt na Farah wafurai Medali.Fahamu zaidi hapa.

 Wanariadha Mo Farah wa Uingereza na Usain Bolt wa Jamaica wameendelea kuitikisa dunia kwenye mchezo huo, baada ya kutwaa medali nyingine za dhahabu.
Wakati Farah, mzaliwa wa Somalia aliyekimbilia Uingereza kukwepa machafuko akizoa medali ya dhahabu kw akukimbia umbali wa mita 5,000 kwa Dakika 13:50.38, Bolt alipata dhahabu ya 11 baada ya kushinda kwenye mbio za kupokezana vijiti kwa watu wanne umbali wa mita 100.
Huu ni ushindi wa tatu mfululizo kwa Farah aliyepata pia kutwaa dhahabu kwenye mashindano ya dunia lakini pia kabla kwenye michuano ya Olimpiki. Haikuwa ushindi rahisi kwa Farah, wala hakuongoza muda wote wa mchezo, kwani mshindi wa Kenya kwenye michuano ya Jumuiya ya Madola, Caleb Ndiku aliongoza kwa kipindi fulani.

Hata hivyo, Farah aliongeza kasi na kumpita Ndiku kwenye kona ya mwisho na kujihakikishia medali ya saba ya dhahabu ya dunia. Alieleza furaha yake kwa kutwaa ubingwa lakini zaidi kuweka historia duniani.
Alidokeza kwamba hakuwa anajihisi timamu sana kiafya, kwani misuli ya paja ilionekana kutaka kumharibia mambo lakini jopo la madaktari wake wakamsaidia. Akasema kwamba awali alihisi woga lakini hatimaye mambo yakaenda vyema.
Kwa upande wa Bolt, alifanya vyema na wenzake watatu walipopokezana vijiti na kumaliza mita 100 kwa sekunde 37.36, na kwa Bolt ilikuwa ukamilisho wa dhahabu tatu katika mashindano haya, kwani alitwaa ya kwanza kwenye mbio za mita 100 na kisha mita 200.
Toa maoni yako hapa.

0 comments:

Post a Comment