Friday 28 August 2015

#MICHEZO>>Messi awa mchezaji bora zaidi Ulaya.Fahamu zaidi hapa.

Mchezaji wa Barcelona na Timu ya Taifa ya Argentina, Lionel Messi ametajwa kuwa mchezaji bora wa Ulaya.

Messi ameibuka katika nafasi hiyo baada ya kumzidi mchezaji bora wa dunia anayemaliza muda wake, Cristiano Ronaldo wa Real Madrid na Ureno na Luis Suarez ambaye Messi alishirikiana naye vyema Barcelona msimu uliopita. Suarez ni mshambuliaji wa kimataifa wa Uruguay.

Kura ya kutafuta mchezaji bora wa Ulaya iliendeshwa mubashara na wanahabari Alhamisi hii ikijumuisha nchi zilizo katika Shirikisho la Soka la Ulaya (Uefa). Messi amepata kuwa mchezaji bora wa dunia mara nne, ambapo yeye na Ronaldo wanafungana kwa idadi ya mabao 77 katika UCL.
Toa maoni yako hapa.


0 comments:

Post a Comment