Saturday 22 August 2015

#YALIYOJIRI>>>SHERIA MTANDAO YASIYOTAJWA ITAKAPO ANZA KUTUMIKA SEPTEMBA MOSI.



Na Yusuph Kileo Zikiwa zimebaki siku chache kuanza kutumika kwa sheria mtandao Nchini Tanzania, Mengi yame endelea kuzungumzwa ikiwa ni pamoja na kurudia mapungufu yaliyopatikana katika sheria ya awali iliyo wasilishwa bungeni na kusambazwa kwa maneno kua sharia hii mtandao ipo kuziba watanzania midomo huku wengine wakizungumzia itakiuka faragha za watanzania. Sheria hii inakuja kusaidia mambo mengi na ni wazi mengi hayo yamekua hayazungumzwi kabisa. Hivi karibuni kupitia mkutano mkuu wa mwaka wa maswala ya usalama mitandao ambapo moja ya mijadala iliangazia sharia hii na kutolea ufafanuzi yale yaliyokua hayajaeleweka vizuri. Binafsi Nilikua mmoja wa washiriki ambapo kwa ujumla wetu tulianisha mambo kadhaa na kuzidi kutoa hofu kwa yale ambay yameendelea kupotoshwa kuelekea matumizi ya sharia hii mtandao. Makala hii itajikita kwenye hayo yasiyo zungumzwa kwa wingi hivi sasa. Upotevu wa fedha, hivi karibuni akizungumza na Jeshi la polisi waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa alitahadharisha kua shilingi trilioni 54.4 zitakuwepo kwenye hatari ya kuingia katika mikono ya wahalifu wa mitandao, endapo Sheria za Mitandao na Miamala ya fedha haitatumika. Alianisha kua fedha hizo ni sawa na trioni 4.4 kila mwezi. Profesa Mbarawa amesema fedha hizo lazima zilindwe  kwa kuwekewa sheria zenye kuzuia na kutoa adhabu kwa watu watakaoingilia mihamala ya fedha. Kuzilinda fedha hizo Sheria mtandao haina budi kuwepo ili kuwapa uwezo wahusika kufanya kazi yao ipasavyo.
Chanzo
                               Michuzi

0 comments:

Post a Comment