Sunday 30 August 2015

#MICHEZO>>KOMBE LA DUNIA LA VIJANA.Fahama yaliyojiri hapa.

*Mali, Senegal robo fainali
*Nigeria watolewa na Ujerumani
Michuano ya Kombe la Dunia kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 20 imefika patamu, ambapo Mali na Senegal wameingia robo fainali.
Mali waliwashangaza Ghana waliokuwa wakipewa nafasi kubwa ya kusonga mbele kwa kuwachabanga 3-0 mabingwa hao wa 2009.
Kwenye kundi lao la B Ghana waliwafunga Argentina na kuwa juu hivyo kupewa nafasi kubwa ya kuingia robo fainali.
The Eaglets waliuanza mchezo kwa nguvu na wakafanikiwa kuwaibua washabiki wao vitini katika dakika ya 20 tu pale Diadie Samassekou alipokwamisha kombora nyavuni baada ya kugongeana haraka haraka na Adama Traore.
Baada ya mapumziko walipata bao la pili kupitia kwa Diedonne Gbakle, aliyekatiza kutoka upande wa kulia, akawalamba chenga wachezaji wawili wa Ghana na kuachia fataki na kuzama chini tu ya mtambaa wa panya.
Ghana walishaona Jua limewachwea na wakati wakijaribu bila mafanikio kurudia hali yao ya zamani, walipachikwa bao jingine dakika tisa kabla ya mpira kumalizika, kwa bao la Aboubabacar Doumbia aliyewatoka walinzi wa Ghana na kuweka kitu kwenye kona ya goli.
Senegal nao walifanikiwa kuingia hatua ya robo fainali baada ya kuwafunga Ukraine kwa mikwaju ya penati, kwani katika muda wa kawaida walikwenda sare ta 1-1, shujaa wa mechi akiwa kipa Ibrahima Sy.
Licha ya kuingia katika muda wa ziada, walibakia nguvu sawa, mabao yakiwa yamefungwa na Artem Biesiedin’ dakika ya 77 na kusawazishwa na Sidy Sarr dakika ya 83.
Katika changamoto ya penati, Senegal walishinda.
Toa maoni yako hapa.

0 comments:

Post a Comment