Tuesday 25 August 2015

#MICHEZO>>>>JUAN QUADRADO NAYE AUNGISHWA JUVENTUS.

Katika hatua nyingine, winga wa Chelsea, Juan Quadrado aliyeshindwa kuonesha makali kwenye msimu wake wa kwanza Stamford Bridge ameelekea Torino, Italia kwa ajili ya kujiunga na Juventus ikiwa atafuzu vipimo vya afya.

Quadrado, 27, ambaye ni mchezaji wa kimataifa wa Colombia alipokewa uwanja wa ndege na viongozi wa klabu hiyo, ikiwa ni miezi sita tu tangu ajiunge Chelsea kwa ada kubwa ya pauni milioni 23.3 kutoka Fiorentina na sasa anatarajiwa kukipiga na mabingwa hao wa Italia.

Quadrado alicheza mechi 15 tu kwa Chelsea, ambapo ni mara nne tu alianza tangu dakika ya kwanza. Kocha Jose Mourinho amekuwa akionesha dalili za kutaka kumtoa kwa mkopo, akijilaumu pia kwa kitita kizito alichotumia kumsajili bila yeye kulipa fadhila uwanjani.

Chelsea walimsajili winga wa Barcelona, Pedro Rodriguez kwa pauni milioni 21.1 Alhamisi hii na tayari katika mechi yake moja ameonesha cheche, akifunga bao na kusaidia kupatikana kwa jingine.
Pamoja na viongozi, Quadrado alipokewa na washabiki na yeye akasema kwamba Juventus ni klabu kubwa inayoheshimika kote duniani na kwamba angependa kuanza kuitumikia kwa nguvu.

0 comments:

Post a Comment