Monday 31 August 2015

#MICHEZO>>>De Bruyne atua Man City.Fahamu zaidi hapa.

 *Januzaj ajiunga na Borussia Dortmund
*Javier Hernendez aenda Bayer Leverkusen
*De Gea atua Real Madrid
*Man U wamnasa Martial kutoka Monaco
* Borini njiapanda, Jelavic ni West Ham
Hatimaye Manchester City wamekamilisha usajili wa kiungo waliyekuwa wakimsaka kwa udi na uvumba, Kevin De Bruyne kutoka Wolfsburg, kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni 55.

De Bruyne, 24, amesaini mkataba wa miaka sita Etihad na anakuwa mchezaji wa nne mkubwa kusajiliwa kiangazi hiki, baada ya Raheem Sterling kutoka Liverpoo na Timu ya Taifa ya England, Fabian Delph wa Aston Villa na mchezaji wa kimataifa wa Argentina, Nicolas Otamendi aliyekuwa Valencia.

De Bruyne ni mchezaji wa kimataifa wa Ubelgiji, ambaye anakuwa wa pili aghali katika usajili kwa klabu za England, nyuma ya Angel Di Maria aliyesajiliwa kiangazi kilichopita na Manchester United kwa pauni milioni 59.7 kutoka Real Madrid, akashindwa kung’ara na sasa ameuzwa Paris Saint-Germain (PSG).

Kocha wa Manchester City, Manuel Pellegrini alionesha furaha yake kumpata mchezaji huyo, na alikuwa na haya ya kusema kumhusu: “Inabidi uwe na mchezaji wa kipekee ili kuboresha kikosi. Sisi hupenda mchezo wa kushambulia sana na unaovutia, kwa hiyo kusajili mchezaji kama huyu utakuwa msaada mkubwa sana kwetu. Ana kila tunachohitaji – utimamu wa mwili, akili, ufundi na mbinu zinazotakiwa uwanjani.”

De Bruyne aliyekuwa Chelsea kabla ya kutupwa kwa madai hana kiwango, amesema anataka kufika katika kilele cha mafanikio kwa maana ya kiwango cha juu cha uchezaji soka huku akiwapatia klabu yake mataji. Amepewa jezi
Picha zaidi hizi hapa.





0 comments:

Post a Comment