Monday 31 August 2015

#YALIYOJIRI>>>Zantel yaingia ubia na Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) kutoa huduma za kibenki kupitia simu za mkononi.Fahamu zaidi hapa.

 Waziri wa Fedha wa Zanzibar, Mheshimiwa Omari Yusuf Mzee, akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa huduma ya Benki yako Kiganjani ya Zantel pamoja na benki ya PBZ. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Zantel, Pratap Ghose, akifuatiwa na Mwenyekiti wa bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Salmin Senga, na mwisho kulia ni Mkurugenzi wa benki ya PBZ, Juma Mohammed.
  Mkurugenzi wa Zantel, Pratap Ghose akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma mpya kati ya kampuni yake na benki ya PBZ, Benki Yako Kiganjani.
 Mkurugenzi wa Huduma ya Kifedha za simu za mtandao, Hashim Mkudi akielezea namna ya kutumia huduma ya Benki Kiganjani Mwako iliyozinduliwa kwa ushirikiano wa kampuni yake na benki ya PBZ.
Mkurugenzi wa benki ya PBZ, Juma Mohammed akizungumza wakati wa kuzindua huduma ya Benki Kiganjani Mwako, inayoendeshwa na kwa ushirikiano wa benki yake na kampuni ya Zantel.

0 comments:

Post a Comment