Sunday 13 September 2015

#YALIYOJIRI>>John Magufuli akiwa kwenye kampeni Igunga.Fahamu zaidi hapa.

  Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM,Dkt Magufuli akiwasalimia maelfu ya Wananchi waliofika katika uwanja wa Barafu mjini Igunga,Dkt Magufuli aliwahutubia wananchi hao.
 Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Magufuli akisisitiza mbele ya maelfu ya Wakazi wa mji wa Igunga jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara kuwa Serikali ya awamu ya tano itajenga viwanda mbalimbali vikiwamo viwanda vya nguo ikiwa ni mkakati wa kuinua zao la pamba ambalo linalimwa kwa wingi mikoa ya kanda ziwa,amesema kuwa Serikali yake imedhamiria kuleta mabadiliko bora na si bora mabadiliko na kuongeza kazi kubwa atakayofanya ni kusimamia vema rasilimali za nchi kwa maslahi ya Watanzania wote.
 Dkt Magufuli kwa nyakati tofauti kwenye mikutano ya hadhara akiwa katika wilaya ya Maswa na kisha jimbo la Kishapu na Igunga, Dk.Magufuli amesema kuwa anatambua umuhimu wa kuwa na viwanda nchini na hivyo serikali yake itasimamia ujenzi wa viwanda kwa lengo la kuimarisha uchumi na wakati huo huo kusaidia wakulima na wafugaji kunufaika na shughuli wanaofanya nchini.   
Toa maoni yako hapa.

0 comments:

Post a Comment