Saturday 26 September 2015

#YALIYOJIRI>>>Mtu mmoja amekufa papo baada ya TASHRIFF kuligonga gari dogo.Fahamu zaidi hapa.

Mtu mmoja amekufa papo hapo na wengine wanne wamejeruhiwa vibaya baada ya basi la kampuni ya TASHRIFF lililokuwa likitokea Tanga kwenda Dodoma kuligonga gari dogo aina ya Nissan Safari katika eneo la kange jijini Tanga.
Akizungumza katika eneo la tukio dereva wa gari dogo ANDREW LIMONGA amesema dereva wa basi la TASHRIFF,MOHAMED JUMAA ambaye ndiye pekee aliyefariki dunia katika ajali hiyo hakufunga mkanda.
Amesema basi la TASHRIFF liliigonga gari yale kwa nyuma na alipoyumba akagongwa tena upende wa kulia ndipo magari yote mawili yalipoteza mwelekeo na kuanguka.
 Chanzo
                                           ITV HABARI

0 comments:

Post a Comment