Sunday 4 October 2015

#YALIYOJIRI>>>Kingunge Kwanzia sasa mimi najitoa katika chama cha mapinduzi.Fahamu zaidi ujue alichokisema.




Hotuba ya Kingunge
  Nimekua ccm kwa jumla miaka 61,na nimetumikia naamini kwa uaminifu.

Nimetumikia chama changu kwa nyazfa mbalimbali,kwa kukijenga na kukiimarisha.

Kwa bahati nzuri baba wa taifa alinieka karibu nae,hasa ktk nyanja ya FIKRA.
Vyama vya TANU NA AFRO tulivyovijenga vilikua vya kupigiania ukombozi.

Kwenye CCM mi ni mmoja wa waanzilisha,na kwa TANU si mmoja wa 17 ila ni miongoni mwa wanachama wa mwanzo.

CCM tuliijenga ili iwe bora kuliko vyama viwili vilivyoiunda.
Haswa Kuwe na demokrasia ndani ya chama.

Mchakato wa kumpata wagombea watano ambao kamati kuu ingependekeza kwa halmashauri kuu ulikua na matatizo ya kimsingi.

Mchakato wenyewe ni BATILI.

Swala la watu kugombea urais si jipya,tulianza mwaka 1995.

Mimi ktk historia yangu,pale ninapoona katiba inachezewa ama inakusudiwa kuvunjwa,nimekua na tabia ya kusema waziwazi kwamba si sawa.

Mimi sikubaliani na kilichotokea katika chaguzi mwezi aug,na udhalilishaji wa baadhi wenye sifa wakaulizwe maswali na kamati kuu.

kilichofanyika katika mchakato wa uchaguzi CCM NI ukiukwaji wa katiba.

Wengine wanayumba sasa hivi,kwa sababu hawajui haki zao,na kama wanazijua hawana ujasiri wa kujitetea.

Wengine tuliingia chama hichi si kutafuta cheo wala fedha.

Sisi wengine katika chama tulitafuta chombo cha ukombozi wa Watanzania.

kwakua chombo chenye madaraka kimeamua kubinafsisha chama.
Kwa maslahi ya sijui nani.
Na mambo yanafanyika ya ajabu.
Vijana wanatumiwa kudhalilisha watu wazima
Mavuvuzela wanaajiriwa kutukana watu

Mimi sikubali na hiki si chama tulichokubaliana kukijenga
Na mimi kwanzia leo naachana na chama cha mapinduzi.

Siwezi kukaa katika chama kisichoheshimu katiba,
Kwanzia sasa mimi najitoa katika chama cha mapinduzi.

Najua uamuzi utawasumbua baadhi ya makada na wazee wenzangu,ila ni uamuzi ambao lazima niufanye kwasababu vinginevyo nitajisaliti mwenyewe.

nimehusika kuweka misingi ya chama kwasababu tuliamini ni misingi sawa.na kuhakikisha ndani ya chama kunakua na demokrasia.

Nawachia CCM pili sikusudii kujiunga na chama kingine chochote, nina sababu nimekua mwanaharakati ktk tanu hadi ccm kwa miaka 61.

"La tatu mimi ni raia tena raia huru niliye na haki zangu, za kisiasa na za kijamii, hivyo nitaendelea kuwa na msimamo kuhusiana na maswala ya Nchi yangu....."

nitaendelea kuwa na misimamo katika masuala yahusiyo nchi yangu_kingunge

kuna msemo unasema kidumu tawala ina maana wanamaanisha hakuna mabadiliko



0 comments:

Post a Comment