Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Abdallah Pazi ‘Dulla Mbabe’, juzi Jumamosi alijikuta akipoteza pambano lake la Ubingwa wa Dunia (WBC) dhidi ya Mjerumani Toni Kraft licha ya kudaiwa kumpiga mpinzani wake vya kutosha.
Katika
 pambano hilo la raundi kumi lililofanyika kwenye Ukumbi wa Ballhaus 
Forum, Munich, Ujerumani, Mbabe alionekana kumdhibiti vilivyo Mzungu 
huyo kwa kumpelekea makonde mazito kabla ya kumdondosha chini katika 
raundi ya tatu kufuatia kumchapa konde kali la mkono wa kulia, hali 
iliyosababisha ahesabiwe mpaka kumi lakini aliweza kuokolewa na kengele 
ya mapumziko.
Baada 
ya kipondo hicho, Mzungu huyo alianza kucheza kwa kukimbia muda mwingi 
ulingoni huku akipokea ‘vikombe’ kutoka kwa Dullah Mbabe hadi kumaliza 
raundi kumi na majaji wawili kumpa ushindi Mjerumani huyo hali 
iliyosababisha mashabiki waliojitokeza kwenye pambano hilo kuamini kuwa 
Mzungu mwenzao hakustahili kushinda pambano hilo.
Akizungumza
 mara baada ya pambano hilo moja kwa moja kutoka katika Jiji la Munich, 
Ujerumani, Mbabe alisema amesikitishwa na matokeo hayo, kwani majaji 
walimpendelea mpinzani wake, licha ya kumpiga katika raundi zote.
“Kiukweli
 nimepoteza pambano langu kimizengwe, majaji wamempa mpinzani wangu 
ushindi wa jumla kwa tofauti ya pointi mbili, kitu ambacho kimepingwa 
hata na mashabiki wa ngumi huku Ujerumani, wengi wao ni Wazungu, kwa 
kuwa kila mtu ameona nilivyokuwa namshughulikia bondia wao.
 “Nilimpiga
 ngumi kali ya kulia akaenda chini lakini alihesabiwa mpaka nane na 
akaweza kuendelea na pambano kwa ujanja kwani muda mwingi nilikuwa nampa
 vitasa vizito,” alisema Mbabe.













0 comments:
Post a Comment