Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya CHADEMA, Godbless Lema leo amefikishwa mahakamani mkoani Arusha na kusomewa shtaka la uchochezi kwa viongozi wa serikali.
Lema amefikishwa leo mahakamani akiwa tayari amekaa rumande takribani siku 7 tangu alipokamatwa.
Lema
 anakabiliwa na shtaka la uchochezi ambapo ni pamoja na kumtishia Mkuu 
wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na kauli yake aliyoitoa dhidi ya Rais 
Dkt Magufuli kuwa Mungu amemuonyesha asipojirekebisha atafariki.
Baada
 ya kusomewa shtaka hilo, Lema amerejeshwa rumande baada ya kukosa 
dhamana kufuatia pingamizi lililowekwa na upande wa Jamhuri.
 










 




 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment