Thursday 25 May 2017

Baada ya Rais Magufuli Kufichua Ufisadi Mkubwa wa Serikali ya Awamu ya Nne na Tatu Jana..Afande Awataka Mkapa na Kikwete Kutubu.

Msanii wa muziki wa bongo fleva, Afande Sele amefunguka na kusema kama angekuwa ni mmoja kati ya Rais wa awamu ya tatu au awamu ya nne basi angekaa kimya na kujifungia ndani huku akitubu na kuwaomba radhi wananchi kwa mambo waliofanya.
Afande Sele ambaye pia ni mwanasiasa aliyegombea ubunge jimbo la Morogoro Mjini kupitia ACT Wazalendo, amesema hayo siku moja baada ya Rais John Pombe Magufuli kupokea ripoti ya uchunguzi wa madini ambayo imeonyesha kulikuwa na wizi mkubwa jambo lililopelekea Rais kumtengua Prof. Muhongo katika nafasi yake ya Waziri wa Nishati na Madini.
"Baada ya kupata matokeo ya taarifa ya tume iliyoundwa na Rais Magufuli kuhusu usitishwaji wa kusafirisha mchanga wa madini kwenda nje ya nchi. Nimechoka mwili na akili kwa jinsi kama taifa lenye mamilioni ya watu masikini sana tulivyokuwa tunapoteza mabilioni ya dolla kikatili kabisa kwa makusudi ya watanzania wenzetu wachache tena wale tuliokua tumewapa dhamana kuu za kutuongoza." alisema Afande Sele
Afande Sele alizidi kusisitiza kuwa viongozi hao wanapaswa kuomba radhi kwa wananchi kwa madudu ambayo wamefanya kipindi cha utawala wao 
"Kwa sababu uso umeumbwa na haya na kwa sababu mimi siyo mwanahizaya. Laiti kama mimi ningekua ni mmoja kati ya watu hawa daima ningefunga mdomo wangu, ningejifungia ndani kwangu, ningetubu kwa Mungu wangu, ningewaomba msamaha wananchi wenzangu kwani wametia aibu wanapaswa kutubu" alisema Afande Sele


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment