Saturday 20 May 2017

Mpenzi wa Rayvanny arudisha mwili wake wiki kadhaa baada ya kujifungua mtoto wa Kiume.

Fahyma ambaye ni mpenzi na mama ya mtoto wa Rayvanny amekuwa akiwaekea mashabiki wake picha huku akionesha umbo lake ambalo limerudi wiki kadhaa baada ya kujifungua mtoto wake wa kwanza, Jaydan.

Mrembo huyu ambaye amejitambulisha kama teen mom amewapa wengi nafasi ya kufikiria kuwa bado hajafikisha miaka 20 na ikiwa ni ukweli basi inaonekana kuwa ameharakisha maisha yake.

Hata hivyo Rayvanny bado anampenda kulingana na mambo ambayo huyaweka kwenye mtandao wake wa Instagram. Tukiyaacha hayo, picha ambazo Fahyma ameziweka zinamuonesha kama amevalia nguo za kuogelea na kwa kweli amependeza sana.
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment