Saturday 20 May 2017

MREMBO Auawa na Kuzikwa Kama Mbwa.

Dada mrembo kutoka Kenya Nairobi Claire Njoki Kibia aliyekuwa akifanya kazi ya ujambazi Kwa kutumika ktk kutega wanaume na wakati mwingine yeye mwenyewe kwenda frontline, ktk kufanya ujambazi, aliuawa mapema wiki hii na kuzikwa Kama mbwa. 
Mrembo huyo alisumbua Sana enzi za uhai wake, hakuna mkenya ambaye hakuwa anajua habari za Claire.
Inadaiwa marafiki zake wengi waliogopa kwenda Kwa hofu ya kukamatwa na police maana rafiki zake wengi ni majambazi Sugu.
Inasemekana hata waliohudhuria msiba huo hawakuwa na uchungu wowote na wengi walikuwa majirani. 
Mara baada ya mazishi ,baadhi ya waombolezaji ambao walisemekana kuwa ni majambazi wenzake na Claire walikamatwa na askari kanzu waliokuwa pale msibani wakijifanya Kama waombolezaji wengine. 
"Laleni chini au la tunawapiga risasi "
Police mmoja aliyekuwa kavaa kiraia alisikika akitoa amri huku akiwa kawanyoshea bastola watuhumiwa.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment