Friday 26 May 2017

Everton kutua Bongo Julai, Je ni Simba au Yanga kucheza nao?.

Kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter wa klabu ya soka ya Everton, umethibitisha kuwa klabu hiyo kuwasili nchini mwezi Julai na itakuwa ni timu ya kwanza inayoshiriki Ligi kuu nchini Uingereza kucheza na timu za Afrika mashariki.
Ujio wa Everton ni sehemu ya maandalizi ya msimu ujao wa ligi, Vilabu vinavyo tarajiwa kunufaika na ujio huo ni vile ambavyo vipo chini ya udhamini wa kampuni ya Michezo ya kubashiri ya SportPesa. Kwa hapa nchini mpaka sasa kampuni hii imeingia mkataba na klabu tatu ambazo ni Simba SC, Yanga SC pamoja na Singida United .

Kwa mujibu wa Kampuni ya SportPesa, wameandaa ligi ijulikanayo kama SportPesa  Super Cup , inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi tarehe 5  / 6 / 2017, kwa kushirikisha jumla ya timu 8  kutoka mataifa mawili, Tanzania na Kenya, na mshindi wa mashindano hayo atacheza na timu inayoshiriki ligi kuu nchini Uingereza.
Mshindi wa michuano hiyo mikubwa atapata kiasi cha Dola za kimarekani Elfu thelathini (USD 30,0000) na mshindi wa pili wa michuano hiyo anatarajia kupata kiasi cha Dola za kimarekani Elfu kumi (USD 10,000).
Kutokana na kuthibitisha kwa klabu ya Everton bilashaka mshindi wa mashindano hayo atacheza na klabu hiyo kongwe ilio anzishwa  mwaka 1978.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment